TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - (MDAs &LGAs) - Maelfu Waitwa !

 TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - (MDAs &LGAs)

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - (MDAs &LGAs)
 
Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali na Mamlaka za Serikali za Mitaa (MDAs &LGAs) anapenda kuwataarifu waombaji kazi wote walioomba kazi kuwa usaili wa kuandika unatarajiwa kuendeshwa kuanzia tarehe 14 - 15 Januari, 2023 katika kanda nne (4) za Dodoma, Mbeya, Mwanza na Dar es Salaam. Usaili utafanyika pia Zanzibar.

Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-

i. Usaili utafanyika 14 hadi tarehe 15 Januari, 2023 kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili; muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada;

ii. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa Barakoa (Mask);

iii. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;

iv. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha kazi, Kitambulisho cha Uraia au Hati ya kusafiria;

v. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa, kidato cha IV, VI, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji;

vi. Wasailiwa watakaowasilisha“Testimonials”, “Provisional Results”, “Statement of results”, hatiza matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI;

vii. Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi;

viii. Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili;

ix. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA);

x. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakukidhi vigezo. Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji ya tangazo husika;

xi. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma wanapaswa kuja na vyeti vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni za kufanyia kazi; na

xii. Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wahakikishe wanaingia kwenye akaunti zao na kunakili namba ya mtihani kwa kuwa namba hizo hazitatolewa siku ya usaili.

SOMA MATANGAZO HAYA RASMI KWA UKAMILIFU , KUPITIA LINK ZIFUATAZO :-

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad